Home » » Juma Nature:Nilijisomesha kwa kuuza chuma chakavu

Juma Nature:Nilijisomesha kwa kuuza chuma chakavu

Historia yoyote huwa na msingi wake. Uwe wa kitu au mtu, historia hujengeka kutokana na matukio iwe ya kusikitisha, kusisimua, kufariji hata kutia moyo.
Inaweza kuishia ikihuzunisha, kufurahisha hata kuonyesha ushujaa kutokana na mtiririko wa matukio kwa jambo au mtu husika anayelezea au kusimulia historia yake.
Ndivyo ilivyo pia kwa msanii wa muziki wa kizazi kipya aliyejizolea umaarufu nchini hata nje ya mipaka ya Tanzania kutokana na umahiri wake katika muziki.
Hata hivyo, siyo kila mmoja anajua historia ya nguli huyo katika muziki huo, hata kumfanya apachikwe majina mengi na mashabiki wake.
Mara zote mashabiki hawakusita kufurika alipofanya uzinduzi wa albamu zake. Hiyo huwa ndiyo kile kinachoitwa na vijana kuwa ni habari ya mjini.
Hali hiyo husababisha ulinzi wa ziada kuhitajika ili kudhibiti msongamano wa mashabiki ambao usalama wao kuwa shakani kutokana na msongamano.
Katika mahojiano na mwandishi wa makala haya Nature anaanza kwa kueleza kuwa yeye ni mzaliwa wa jijini Dar es Saam katika Hospitali ya Ocean Road mwaka 1980 na kwamba jina lake halisi ni Juma Kassim Ally.
Anasema kwamba kabla ya kufikiria kuwa mwanamuziki alikuwa ni mchezaji mzuri wa soka katika timu za uswahilini  maarufu kwa jina la ‘Cha ndimu’.
Anaeleza kuwa pamoja na kucheza soka katika timu ndogo wakati huo akisoma Shule ya Msingi Kurasini, alikuwa akiwaza kuwa kipaji hicho cha soka ndiyo ‘kingemtoa’ na kumsaidia maishani.
Anabainisha kuwa alisoma shule ya msingi kwa shida na baada ya kumaliza hakuchaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari.
“Elimu ya ‘kibongo’ bila kuwa na mpango mbadala wa masomo ya ziada, ni vigumu kufaulu. Wenzangu waliokuwa na uwezo walisonga mbele mimi nikaishia hapo, “anasema Nature.
Anafafanua kuwa kutokana na familia yake kutokuwa na uwezo wa kumsomesha, binafsi alikuwa na moyo wa kusoma na  aliazimia kufanya analoweza ili ajiunge na sekondari mwaka unaofuata, baada kusota nyumbani kwa mwaka mmoja baada ya kumaliza elimu ya msingi.
Share this article :
 
Copyright © March 2012. MARIDADI AGENCY
-Haki zote zimehifadhiwa
- All Rights Reserved
Template Modified by Hassan Moh Toziri
Published by Maridadi Agency