Home » » Rais Michael Sata kuzikwa rasmi.

Rais Michael Sata kuzikwa rasmi.



Mazishi ya kitaifa yanafanyika nchini Zambia kumuaga hayati Rais wa nchi hiyo Michael Sata aliyefariki hospitalini mjini London Uingereza mwezi jana.
Sata alikuwa na umri wa miaka 77.
Katika wiki chache zilizopita, wanachi wamekuwa wakitoa heshima zao za mwisho kwa kiongozi huyo ambaye mwili wake ulikuwa umelazwa katika majengo ya bunge.

Mazishi yanayofanyika mjini Lusaka yatahudhuriwa na viongozi mbali mbali wa kikanda.
Rais Sata atazikwa katika eneo lenye makaburi yaliyotengewa Marais wa nchi hiyo.
Taifa hilo kwa sasa linaongozwa na kaimu Rais huku uchaguzi mkuu ukipangwa kufanyika katika muda wa miezi michache ijayo.
Share this article :
 
Copyright © March 2012. MARIDADI AGENCY
-Haki zote zimehifadhiwa
- All Rights Reserved
Template Modified by Hassan Moh Toziri
Published by Maridadi Agency