Home » » UMUHIMU WA MATANGO

UMUHIMU WA MATANGO



WATAALAMU wamesema kwamba matango ni chakula muhimu sana katika mwili wako kutokana na kufanhyakazi mbalimbali za kuuweka sawa pamoja na kuupa maji.
Ni vyema kuhakikisha kwamba kila siku unakula tango kwa afya yako.
Hakika kama upo bize sana kiasi cha kusahau kuinywa maji ya kutosha, kula tango ambalo asilimia 90 ni maji. tango litakuongezea maji unayohitaji.
Tango pia linakabiliana na joto nje na ndani ya mwili. ndio kusema kwa kula tango mwili unapunguza mashambulio ya kiungulia. Pia kama utajipaka tango utapata nafuu sana dhidi ya miale ya jua.
Kazi nyingine ya tango ni kupunguza sumu katika mwili, maji yote yaliyomo ndani ya tango linafanya liwe kama fagio la kuondoa sumu mbalimbali mwilini na ulaji wa kila mara wa tangu unasaidia kuondoa mawe katika figo (kidney stones).
Aidha tango linasaidia kukupatia vitamin.Tango lina vitamin nyingi zinazohitajika katika mwili kwa siku. Kuna vitamin A,B,C ambazo hupiga busti katika mfumo wako wa kinga kukupa uangavu na nishati unayoihitaji.
unaweza kufanya jusi ya tango kuwa na nguvu zaidi kw akuichanganya na karoti na spinachi.Usimenye tango lioshe na kulila na unaposaga kupata juisi vivyo hivyo kwani ngozi yake inavitamini C kiasi cha asilimia 123 ya inayohitajika kila siku katika mwili.
Share this article :
 
Copyright © March 2012. MARIDADI AGENCY
-Haki zote zimehifadhiwa
- All Rights Reserved
Template Modified by Hassan Moh Toziri
Published by Maridadi Agency