Home » » Mikoba ni sehemu ya urembo wa mwanamke

Mikoba ni sehemu ya urembo wa mwanamke




Pindi uwapo katika safari zako,utaona jinsi wanawake wanavyobeba mikoba ya aina mbalimbali.
Wakati mwingine mingi ya mikoba huwachukiza na wengine huwa kichekesho na ingawa wengine urembo wao huambatanishwa na kujipachika tu, vitu maarufu kama vipima joto kwa lugha ya kileo.
Ukiangalia hasa mijini hakuna kabati la nguo la mwanamke ambalo litakosa mikoba, tena ya aina mbalimbali. Kwa mwanamke kuwa na mkoba moja si sawasawa, kwa wale wanaokwenda na wakati kuwa na aina nyingi ya mikoba hii hutokana na ukweli kuwa mikoba hiyo ni sehemu ya mavazi na huambatana na si tu aina ya pamba iliyopigwa bali aina ya viatu vinavyompa kampani mwanamke.
Mwanamke ni kiumbe mrembo kabisa na jinsi anavyozidi kumechisha vitu anatakiwa kuwa mrembo na mwangalifu zaidi kwani anahitaji kujiweka katika kiwango kinachostahili katika kazi zake na uonekano wake.
“Mavazi yako unayovaa yanaweza kabisa kubadili maisha yako” anasema Trinny Woodall mmoja ya watu ambao wako makini kabisa na masuala ya unadhifu wa wanawake wa wanawake katika mitoko ya aina mbalimbali aliyeko Afrika Kusini.
Inakuwaje unapokuwa na vazi tofauti na mkoba wako wa kwapani na ndiyo huo mkoba mmoja pekee unaotumia kwa kwenda pati, kwenda safari. Kwenda kazini na kadhalika?
Hakika kwa mwanamke anayejijali, anatakiwa kuwa na mikoba ya aina tofauti kwa kuzingatia haja ya shughuli zake na pia mavazi yake.
Unachotakiwa siku zote si tu kuwa na mikoba mingio, najua unaweza kuwa na mikoba, unaoupenda lakini ni dhahiri kwamba mikoba hiyo unatakiwa lakini ni dhahiri kwamba mikoba huyo inatakiwa kuwa na mwendo sawa na mavazi yako ili kukupa kitu bomba kinachoweza kuwafanya wanaume wakutazame mara mbili mbili na wanawake wenzako wakuonee gere.
Nina sababu ya kukuambia hivyo lakini wapo wanawake waliojaza mikoba kibao lakini hawaitumii lakini hapo mwanzao waliponunua walijua kwamba ni mikoba bomba kabisa yenye mvuto wa kimapenzi hasa.
Kitu cha kwanza kuzuia ni ule ufujaji wa kununua mabegi yasiyotakiwa, yaani ni kuwa makini na haja yako mwenyewe na mapenzi yako na namna wewe mwenyewe ulivyo.
Ndiyo kusema mkoba lazima uzinagatie mwili wako, upenzi wa maisha yako.
Watengeneza mikoba wengi wanaonya kabisa uchukuaji wa mikoba kwa kuiona bomba kumbe hairandani na wewe unayeibeba.
Mathalani wewe ni mrefu na mwembamba, mikoba yenye mduara ni mizuri lakini kama wewe ni mfupi uliyejazia kiasi chake mkoba unaofanana na ule wa mstatili, mrefu kiasi na mweroro ni kiboko yake.

Ningekushauri kabla hujanunua na kuvaa mikoba hiyo hebu jitazame kwanza katika kioo kwani ni lazima ukubali kwamba uko safi ndiyo uchangamke na mtaa, unapokuwa umejiangalia kwenye kioo utapata namna bora namna bora ya muonekano kama vile unavyojaribu nguo kwenye kioo.
Mikoba myembamba iliyobana hasa huonekana kuwa bomba kwao kama wewe ni mwembamba pia na kama unataka mtu kujisahau kwa namna yake katika mwili wako, lakini haitakusaidia sana kwa matiti yako ni madogo na mikono yako haijajaza inavyostahili.
Halafu tazama sana mikanda ya mikoba ina maana kubwa zaidi ni ndiyo maana ni vyema ikazingatiwa urefu wake katika mabega yako kwani kwa vyovyote vile urefu wake utakavyobeba mkoba wako ina kitu inakifanya katika mwisho wake.
Kwa hiyo kama hutaki mushkeri katika maeneo ya juu ya mapaja usitwae mkoba unaofika pale. Wengi wa wanawake hutokea bomba kama mkoba haufiki katika kiuno au juu yake kidogo, kwani kuketi hapo chini inakuwa mambo si poa katikati ya mwili kwa upande wa juu ndiyo haswaa sawa.
Ni muhimu ukitambua ya kwamba ukubwa wa mkoba wako unaambatana na wewe unaeleweka.
Lakini niseme moja tu mikoba mingi huwa bomba kama haijazwi vitu lakini mathalani kama una simu, shajara na vikorombwezo vya uzuri mkoba mwembamba haufai kwani utatuna na kuchukiza.
Mbunifu wa FUNEKA, Tasleem Bulbulia anasema kwamba mtu wa aina hii kwa kulingana na kazi zake na stahili zake za maisha mikoba mipana ni saizi yake. Ndiyo kusema kazi na stahili yako ndiyo pia itazingatia aina ya mkoba unaotakiwa kuwa nao.
Ulishatambua personaliti yako na aina yako ya maisha ni vyema ukatambua ukweli kuwa chagua kulingana na wewe na si yule kwani kivigezo haiwezekani na kwa maisha pia haiwezekani


Share this article :
 
Copyright © March 2012. MARIDADI AGENCY
-Haki zote zimehifadhiwa
- All Rights Reserved
Template Modified by Hassan Moh Toziri
Published by Maridadi Agency