Home » » Haya ndio makosa tufanyao wakati tukizingatia urembo wetu.

Haya ndio makosa tufanyao wakati tukizingatia urembo wetu.



Kuna makosa mengi sana yanafanywa na watu katika juhudi za kubaki mrembo au kusaka urembo. makosa haya mara nyingi yanaleta matatizo makubwa hasa katika ngozi , macho au katika kichwa.
mara nyingi shughuli hizi za urembo wanawake hujikuta ama wanapitiliza au wanafanya kinyume na kutaka matokeo ya haraka na matokeo yake ni msheshe.
Mambo yanayoharibu katika urembo ni pamoja na kutokuangalia fiziki yaani kutofanya mazoezi. Hata kama hakuna mtu ambaye atakuona kuacha kufanya mazoezi, kutojali usafi kunatibua muonekano wako na kuondoa kujiamini.
Kitu kingine ambacho watu huwa hawakijali ni kusafisha na kurekebisha meno yao. Unapotabasamu kitu cha kwanza kuonekana kwa watu ni meno yako. basi jaribu kuyajali kidogo. yasafishe na hakikisha yanapendeza.
Kitu kingine ambacho huwa watu hawajali ni kuhakikisha kwamba mikono yao i safi na isiyokuwa na mikwaruzo. Usisahau kuitia mikono yako losheni na kuweka kucha zako safi na zinazopendeza na rekebisha kucha hizo.
Usizivuruge sana kope zako, jaribu kutafuta kitu kitakachopendezesha kope zako na kama kuna makosa usizigandamize bali weka kinachotengeneza uonekano safi.
Kuwa mwangalifu na vitu unavyotengeneza au unavyodhani vinafaa kw aurembo wako. vingine vina aleji viogope. na ukipata aleji usikimbilie kujaza kitu kingine bali angalia nini na tafuta suluhu yake kwanza.
La maana ni kuwa ni vyema kujaribu kwanza kitu katika kiganja au mkono mahali padogo kabla ya kuanza kutumia inavyostahili hasa kwa bidhaa unazotengeneza mwenyewe.
Share this article :
 
Copyright © March 2012. MARIDADI AGENCY
-Haki zote zimehifadhiwa
- All Rights Reserved
Template Modified by Hassan Moh Toziri
Published by Maridadi Agency