Home » » UZURI WA MAYAI NA NYAMA YA KWARE KATIKA KUKUKINGA NA MARADHI MBALIMBALI.

UZURI WA MAYAI NA NYAMA YA KWARE KATIKA KUKUKINGA NA MARADHI MBALIMBALI.


Katika siku za hivi karibuni ndege aitwae kware ameanza kuwa ndege maarufu katika baadhi ya wafugaji katika nchi yetu na kwa wale ambao walikuwa wakiwawinda porini enzi hizo bado wana imani kuwa ndege huyu hawezi kufungwa kama hatakimbia basi atajiua, lakini kwa wale wanaotaka kumfuga ndege huyu mdogo mwenye mayai matamu ya madoa doa wanaweza sasa inaweza kugeuka chanzo cha mapato na sehemu ya chakula bora kwa familia.
Leo ningependa niingie ndani kuwa nini hasa tofauti ya mayai ya kware na yale ya kuku ingawa taarifa nyingi nilizopata kwenye mitandao na kwinginekoinaonyesha tu kwa habari za watu waliopata kutumia mayai kware na kuona umuhimu wake katika afya na baadhi ya tovuti kuongelea tu kwamba mayai haya ni mazuri yanasaidia kwa afya bado kama watu wanaotaka kueleew inakuwa haikidhi haja kuamani tu yakuwa yana saidia katika afya, nikiwa mmojawapo wa watu ambao niliona yanasaidia watu walikuwa na matatizo mbalimbali ya kiafya wakiendelea vizuri.
 

Na mpaka sasa mimi napenda kukiita hiki chakula bora na sio dawa kama watu wengi waliotumia wakapata nafuu kwa yale waliokuwa yakiwasibu na wale waliokuwa na dhaifu nyingine katika mwili wakarejea afya maridhawa lakini msimano wangu binafsi napenda kutambua mchango wa haya mayai kama chakula bora.

Ndio maana hata Mungu aliamua kuwapa wana waisrael kama chakula kwenye Kutoka 16:13 na mtumishi Daudi anakomelezea kwenye Zaburi 105:40. Sasa kwa kuwa siku zote najua kuwa Mungu hapingani na sayansi kitu wanasayansi wanachofanya nikungudua tu mambo ambayo Mungu ameyaweka kwahiyo ikabidi nitafute kisayansi sasa sisi tunaopenda kuoona na kufanya akili zetu zielewe maana ukielewa jambo kwenye akili yako ni rahisi kufanyia kazi.
 

Katika kutafuta nikasema pamoja na vyanzo vya wataalamu binafsi ningependa kupata vyanzo vilivyo vya kiserekali ambavyo wao hawana upande waliolalia maana hawa wataalamu binafsi wanaweza kuwa na ajenda zao, Na ndipo nilipopata utafiti wa USDA (United State Department of Agriculture) unaonyesha tofauti za mayai haya kwa kina katika category 78 za nutrients zilizogawanya mayai ya kware yana vitu 31 zaidi ambayo ya kuku hayana kabisa wakati yale ya kuku ya kitu kimoja tu ambacho hakiko kwenye ya kware ambacho naomba nikitaje nacho ni Vitamin K (phylloquinone) na katika hizo 45 vilivyobaki vya kware 42 viko juu na vingine hata mara mbili ya zile za kuku, wakati vya kuku ni 3 vitatu ambayo vimezidi vile vya kware.

Faida hizi zote tunaweza kupata kama watu wetu watajiingiza katika ufugaji wa ndege huyu ambaye anapatikana sehemu nyingi unaweza kuanza kidogo kidogo mpaka wakafikia mwengi,na kama unavyooana hapo juu unaweza kutengeneza banda rahisi la mbao laini na wafu na kuanzia hapo, ila wawapo wadogo waweke kwenye box na kuwawekea taa kama ufanyavyo kuku.
Share this article :
 
Copyright © March 2012. MARIDADI AGENCY
-Haki zote zimehifadhiwa
- All Rights Reserved
Template Modified by Hassan Moh Toziri
Published by Maridadi Agency