Home » » ATHARI YA NGOZI KUUNGUA NA JUA

ATHARI YA NGOZI KUUNGUA NA JUA




Kuna  Msomaji ametuma swali akisema kuwa, yeye ni mwaume mwenye umri wa miaka 30 na amekuwa akifanya shughuli zake chini ya mti ambapo licha ya kuwa na jua kali wakati mwingine kunakuwa na upepo mkali, hali hiyo imesababisha ngozi yake kuungua na jua na ngozi yake kukakamaa imekuwa na makunyanzi kiasi cha kumtisha.
Kulingana na tafiti mbalimbali za kiafya, watalaam wanasema kuungua na jua usoni kunalazimisha ngozi kuongeza uzalishaji wa melanin hali ambayo husababisha mtu kuwa na ngozi nyeusi na kuwa kama kahawia (brown).
Pia unaweza kupata ngozi nyeusi au kahawia kama miale ya jua inakuwa inakupiga moja kwa moja usoni kwa asilimia 60 hadi 80.
Vitamin E inaonesha kuwa na uwezo mkubwa wa kuzuia mtu asipigwe na  miale ya jua usoni, vitamin E hupatikana  katika vyakula kama mafuta ya soya, karanga, nafaka, mboga za majani, kini cha yai na nafaka ambazo hazijakobolewa.
Vitamini E husaidia kukua kwa nywele mara mbili ya kiwango cha ukuaji wa kawaida, pia matumizi ya lotion za kuzuia kuungua na jua zinasaidia sana ili kujikinga na miale ya jua.
Aidha kuungua na jua huwapata  watu ambao mara nyingi hufanya kazi zao wakiwa juani  aina nyingine ya ngozi  ni rahisi sana kuathiriwa na jua na zinahitaji ulinzi zaidi.
Pia ni vizuri kama kila moja atachukua tahadhari mapema ili kujilinda na kulinda ngozi yake isipate tatizo hili.
Watu ambao ngozi zao zimeathirika na jua wanatakiwa kuepuka kushinda juani na wanatkiwa kunywa maji mengi na kula mboga za majani na matunda kwa wingi ili kuweza kurekebisha tatizo lililopo.
Kwa wale wenye makunyanzi kabla ya umri wanashauriwa kula vyakula vyenye chumvi au sukari kiasi kwani matumizi makubwa ya sukari na chumvi ni chanzo cha kuwa na makunyanzi.
Ikumbukwe kuwa kuna vuitu vingi ambavyo miili yetu inahitaji ili kuwa na ngozi nzuri kana usingizi wa kutosha, kupumzika, kufanya mazoezi na kula vizuri.
Share this article :
 
Copyright © March 2012. MARIDADI AGENCY
-Haki zote zimehifadhiwa
- All Rights Reserved
Template Modified by Hassan Moh Toziri
Published by Maridadi Agency