Home » , » USAFI KIPINDI CHA UJAUZITO.

USAFI KIPINDI CHA UJAUZITO.



Kipindi cha ujauzito wanawake wengi hujikuta wakiacha kuzingatia hatua mbalimbali za kujitunza ili kubaki warembo, matokeo yake hupoteza mvuto.

Hali hiyo inaweza kuendelea hata baada ya kujifungua na huenda ikawa mbaya zaidi kwa kuwa mara nyingi kipindi hicho mama hujikuta akitumia muda mwingi kumwangalia mtoto.

Kujifungua au ujauzito haiwezi kuwa sababu ya mwanamke kupoteza urembo uliokuwanao awali. Hivyo ni jukumu la mwanamke mjamzito au aliyejifungua kuhakikisha anabaki na mvuto wake ukiwa kwenye kiwango stahiki.

Kuwa mrembo siyo lazima upake vipodozi vyenye kemikali kwani vinaweza kumsababishia madhara mtoto kwa kuwa atatumia muda mrefu akiwa mwilini kwako.

Katika kipindi hiki mama mjamzito au aliyejifungua anatakiwa kuepuka kupaka mafuta, losheni au manukato yenye harufu kali inayoweza kuwa na madhara kwa mtoto hata kumsabishia wakati mgumu katika kupumua.

Ni vyema utumie vipodozi visivyo na kemikali ili kujilinda usipoteze mvuto wako. Pia tumia muda mwingi kufanya mazoezi mepesi yatakayoweza kukusadia kutengeneza umbile (shape), yako na kuifanya ionekane yenye mvuto wa hali ya juu hata ikiwa umetoka kujifungua.

Hakikisha pia kucha zako zinakuwa fupi na safi, hii haimaanishi kwamba huruhusiwi kupaka rangi unaweza kuziremba kwa mtindo wowote unaopenda lakini ziwe katika kiwango ambacho hakitamdhuru mtoto kwa namna yoyote.

Kitu muhimu cha kuzingatia katika kipindi hicho ni usafi na mwonekano wa ndani na nje. Kwa kufanya hivyo, hata mtoto atakuwa katika mazingira salama yanaweza kumtamanisha mtu mwingine kutaka kumshika.
Share this article :
 
Copyright © March 2012. MARIDADI AGENCY
-Haki zote zimehifadhiwa
- All Rights Reserved
Template Modified by Hassan Moh Toziri
Published by Maridadi Agency