Home » , » Inspiration "words"

Inspiration "words"


Kuna tofauti kubwa sana kati ya mtu anayejenga GHOROFA na yule anayejenga Nyumba ya KAWAIDA.
Anayejenga ghorofa anatakiwa achimbe msingi Mrefu kwenda chini kabla hajaanza kuinua ghorofa yake juu. Hivyo wakati huyu mwingine anapokuwa anajenga Nyumba ya kawaida atakapokuwa tayari anakaribia hata kuezeka unaweza kukuta yule anayejenga ghorofa bado yuko kwenye msingi. Ila siku akianza kuinua ghorofa lake kila mtu atashangaa urefu wa juu atakaoenda nao.
Kwenye maisha ndivyo ilivyo - "If want to go so high, you need to go so deep" (Kama unataka kwenda juu sana ni lazima ukubali kwenda chini sana). Ni lazima ufanye kitu cha tofauti kitakochokujengea future imara.
Ukweli ni kuwa Watu wengi wanaokuzunguka wanajenga maisha ambayo ni kama nyumba ya kawaida. Na wewe kama unataka kujenga maisha yanayofanana na ghorofa lazima ukubali kuonekana unachelewa kwenye baadhi ya mambo.
Hii inamaanisha utalazimika kufanya viti vya TOFAUTI na kuwa TAYARI kusubiri. Utatakiwa kuwekeza wakati wengine wanaenda kununua nguo mpya waendane na fashion, utatakiwa kusoma vitabu wakati wengine wanaangalia movie na kupiga stories, utatakiwa uanzishe biashara yako wakati wenzako wamesharidhika na mshahara wanaopata n.k
Unachofanya kuanzia unapoamka hadi unapoenda kulala kitajulisha kama unajenga maisha GHOROFA ama ya KAWAIDA.
Ukijiona unapoteza muda hovyo, ukiingia Facebook/insta ni kusoma umbea tu, unalalamika, unasema utafanya na hakuna unachofanya ujue unajenga maisha ya KAWAIDA tena ni kama nyumba ya UDONGO

Ukitaka kujenga maisha GHOROFA:
Jifunze kitu kipya leo,
Chukua hatua kuelekea Ndoto yako,
Usiwe mtu wa kulalamika bali tafuta suluhisho kwa kila changamoto.

Je,LEO utajiunga na wanaojenga maisha GHOROFA ama wale wanaojenga maisha ya KAWAIDA?

Thanks
Share this article :

1 comments:

PINNED COMMENT said...

It is a huge relief reading such a carefully curated piece. With all the stress in the world right now, you definitely need some MEDICAL MARIJUANA​ ​ in your life.

In order to do so, you need to know HOW TO ORDER WEED ONLINE​ ​ The world needs all the calm and serenity it could use at this moment in time. I must bookmark this to share with my colleagues. Good job mate. Spread Love every chance you get. PEACE

 
Copyright © March 2012. MARIDADI AGENCY
-Haki zote zimehifadhiwa
- All Rights Reserved
Template Modified by Hassan Moh Toziri
Published by Maridadi Agency