Home » » Unyoaji Ndevu

Unyoaji Ndevu

Moja ya matatizo makubwa kwa wanaume ni unyoaji wa ndevu, kitu ambacho
wakati mwingine huwakera wahusika na wao kujiona kama ni wafungwa.
Pengine hili ndilo linalowasumbua watu mpaka wanajisikia vibaya
kuzaliwa wanaume, halafu hataki ndevu na ndevu zinakuja kama
zimepaliliwa vile. Lakini haya ni maamuzi tu ya kimsingi kwani naamini
unyoaji ndevu unaweza kuwa laini na wenye raha kubwa kama utafuata
haya ambayo nataka kukueleza.
Nafahamu mwanamke wako hapendi ndevu anapenda kuwa na kidevu laini
chenye raha yake kukigusa ingawa najua vile vile wapo wanawake
wanaopenda kukwanguliwa kidogo kwa namna Fulani na kidevu chenye
ndevu.
Kwa wanaume wengi asubuhi ni siku ya matatizo makubwa. Ili kuondoa
matatizo haya yafuatayo yanaweza kabisa kukusaidia kukuweka katika
aina Fulani ya raha kubwa.
1.Chagua mashine ya kunyolea na wembe ambao unadhani unaswihi ngozi
yako. Kuna aina nyingi sana za mashine za kunyolea pamoja na nyembe
zake ni muhimu kujua wembe ambao unatumia kwa kuzingatia mahitaji yako
hasa ya aina ya ndevu
2.Weka uso safi na usio uchafu. Safisha kabla ya kunyoa. Hii
inakusaidia kufungua matundu yanayoshikilia ndevu kabla ya kunyoa ili
kuweza kupata mnyoo laini na wenye uhakika.
3. Usisahau kuloweka kidevu chako vyema. Hii inasaidia wenye kupita
kiulaini zaidi na kama unatumia kiwembe cha kawaida basi ni vyema sana
kufanya kazi hiyo ukitoka kuoga.
4.Tumia maji ya moto siyo yanayounguza kama inawezekana, yanasaidia
sana kufungua vishimo vya vinyweleo. Pia unaweza kupata masaji ya
chapchap katika uso ili kusaidia kulainisha kidevu chako.
5.Chagua krimu hasa inayostahili kwako ya kunyolea kwa kutegemea ngozi
yako na chagua linalostahili unalotaka. Jipake kiasi cha kutosha
katika sehemu zinazostahili kwani husaidia kuburudisha ngozi.
6.Unaponyoa chagua zinapoelekea ndevu. Usiendelee kunyoa sehemu
iliyokwisha kunyolewa. Italeta matatizo na ua uwasha na ukomavu wa
aina Fulani wa kidevu na mbaya zaidi unaweza kujikata.
7. Baada ya kujinyoa, osha uso wako na ondoa krimu zote. Tumia
moistrurizer baada ya kunyoa.
Epeka kutumia after shave yenye pombe. Pombe inasababisha ngozi
kupoteza unyevunyevu wake kwa haraka.
Share this article :
 
Copyright © March 2012. MARIDADI AGENCY
-Haki zote zimehifadhiwa
- All Rights Reserved
Template Modified by Hassan Moh Toziri
Published by Maridadi Agency