Home » » Miwani ya jua unayoivaa ni salama kwa macho yako?

Miwani ya jua unayoivaa ni salama kwa macho yako?



Wengi wanapendelea kuvaa miwani bila ya kupata ushauri wa daktari huku wengine wanaamua kuvaa miwani bila kuwa na tatizo lolote kwenye macho yao ili mradi wanaona miwani inawapendeza. Miwani mingi ya macho inatumika bila kuwaona wataalam wa macho hiyo ni hatari kubwa sana kwako.

Leo tunazungumzia kuhusu miwani ya jua. Wengi wanapenda kununua miwani hii mitaani na kuijaribu na kama wanaipenda wanaamua kuivaa.
Kuwe na mvua au jua watu wengi hupendelea kuficha nyuso zao kwa miwani kwa jinsi wanavyotaka.
Unaweza kuwa na miwani yenye fremu nzuri na kioo cha kutia nakshi lakini je uko kwenye vipimo vya macho?

Yaani miwani yako hiyo inakidhi kweli mazingira ya kukukuhami na jua? Vipi shauri wa miwani inayoacha nafasi ya kuhangaika kuangalia juu au chini na wakati mwingine kioo hakifai kabisa, tazama pamoja na urembo huenda ukapata mikunjo ya ngozi na hili hutalipenda.
Kama unaweza pata ushauri wa daktari kama hujaamua kuwa na miwani kwa ajili ya usalama na ulinzi wa macho yako.
Share this article :
 
Copyright © March 2012. MARIDADI AGENCY
-Haki zote zimehifadhiwa
- All Rights Reserved
Template Modified by Hassan Moh Toziri
Published by Maridadi Agency